MIFU,O YA SIASA



SIASA N,UTAMADUNI NA UTANDAWAZI


1. KUCHANGANUA MIFUMO YA SIASA ILIYOPO KATIKA JAMII ILI KUBAINI NA ATAHRI ZAKE.

1. DHANA YA SIASA
Siasa;- ni njia ya kufanya maamuzi katika taifa, mji au hata dunia nzima (siasa ya kimatatifa).
Sehemu muhimu ya siasa ni majadiliano kati ya watu mbalimbali wenye nguvu au mamlaka.
Katika demokrasia kila mtu ana kiasi fulani cha nguvu, kwa hiyo siasa ya demokrasia ina maana ya watu wote kuchangia maamuzi.
2. MIFUMO YA SIASA
Hapa chini, mifumo mingine ya kisiasa huelezwa kifupi:
Utawala wa Kifalme
ni mfumo wa uongozi unaompa mamlaka ya dola na ya serikali Mfalme. Katika mfumo huu madaraka hurithiwa na mtu wa familia ya kifalme.
Utawala wa Kiimla
ni mfumo wa uongozi unaotoa madaraka yasiyo na mipaka kwa kiongozi. Katika utawala huu watu binafsi hawana haki na uhuru katika maamuzi.
Utawala finyu
ni mfumo unaowapa wachache nguvu za maamuzi katika dola na serikali. Nafasi ya wachache hawa hutokana na haiba na uwezo wao kiuchumi, kijamii, kijeshi au kutokana na mafanikio yao katika nyanja mbalimbali za maisha. Mfumo huu ni nadra sana siku za hivi karibuni. Pia waweza kuitwa utawala wa makabaila.
Utawala wa Umma
ni utawala unaotokana na jamii kuamua misingi ya kujiongoza. Mfumo huu wa utawala hujulikana kama Utawala wa Kidemokrasia.
Demokrasia;- kwa asili neno hili limetokana na maneno mawili ya kigiriki ambayo ni  demos  linalo maanisha  watu na kratos linalo maanisha nguvu tawala.kwa maana hiyo demokrasia ni utawala aunguvu ya watu.

Demokrasia ni mfumo  unatoa fursa ya madaraka kwa umma moja kwa moja au kutokana na kuwakilishwa.hivo tunapata aina mbili kuu;-
  1. Kuwakilishwaji
  2. Moja kwa moja(ushirikishwaji wa watu wote)……………….
   na umegawanyika katika sehemu nne.
  1. Demokrasia Baguzi
ni aina ya Demokrasia inayojikita katika kulinda nguvu za kiuchumi zaidi.
  1. Demokrasia Duni
ni aina ya demokrasia inayotokana na makundi ya watu na kisha kupitia makundi hayo watu kuunda serikali mfano: chama - serikali.
  1. Demokrasia Endelevu
ni aina ya demokrasia inayotoa fursa ya usawa na kupinga matabaka katika jamii.
  1. Demokrasia Shirikishi
katika aina hii ya Demokrasia wachache hupewa dhamana na wengi katikauwakilishi wa jamii katika maamuzi.
Wachache uchaguliwa na wengi kwa njia ya Demokrasia huru na haki kwa kufuata Katiba ya nchi hiyo. Mfano: Wabunge uwakilisha wananchi wao katika kuleta maendeleo na kuishauri serikali juu ya maendeleo ya nchi.


.Misingi ya demokrasia.
  • Usawa
  • Uwajibikaji
  • Uchaguzi ulio huru na haki
  • Uhuru wa kiuchumi
  • Utawala wa sheria
  • Vyama vingi vya kisiasa
  • Haki za binadamu
  • Uadilifu.


3.ATHARI ZA MIFUMO YA SIASA KATIKA JAMII-ULIMWENGUNI.
 SWALI;Kuna athari gani  zinazoweza kujitokeza kutokana                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                            na mifumo hii  ya siasa katika jamii na ulimwengu kwa ujumla.
4.DHANA YA DOLA
Dola ( nchi, serikali, taifa; ing. state) ni utaratibu wa kisiasa wa jamii katika eneo fulani.

Ufafanuzi wa "Dola"

Fani mbalimbali huwa na maelezo tofauti kiasi juu ya maana ya dola:
  • sheria hufundisha dola kuwa mamlaka ya jamii ya taifa; ina tabia tatu za kimsingi ambazo ni
    • eneo la dola,
    • taifa au watu wa dola na
    • mamlaka ya dola juu ya watu na eneo lake.
  • elimu jamii hufundisha kufuatana na Max Weber dola kuwa jumuiya au jamii ambayo ina mamlaka ya kukubalika ya pekee katika eneo fulani; hivyo ni uhusiano wa utawala wa watu juu ya watu unaofuata haki na sharia.
  • elimu siasa hufundisha dola kuwa muundo wa mamlaka ya umma kwa ajili ya kuratibu mambo ya umma.
  • falsafa hufundisha dola kuwa utekelezaji wa shabaha za kimaadili za kila mtu na jamii kwa pamoja; Hegel alisema dola ni mwendo wa Mungu katika historia; msingi wake ni akili inayotaka kuwa uhalisia.

Aina za Dola

Dola hutokea kwa maumbo mbalimbali kwa mfano jamhuri au ufalme. Dola inaweza kujitegemea kabisa au kuwa sehemu ya shirikisho au muungano kama Muungano wa Madola ya Amerika. Ndani ya maumbo haya kuna njia mbalimbali za kutekeleza mamlaka na kuratibu serikali kwa mfano kwa njia ya demokrasia au udikteta.

Vyombo vya Dola
Kiini cha dola ni utekelezaji wa mamlaka katika eneo fulani. Hapo kuna chombo kinachoitwa serikali chenye mamlaka haya mkononi. Serikali inaangaliwa na taasisi nyingine.
Katika madola ya kisasa kuna mgawanyo wa madaraka wa dola kwa taasisi mbalimbali:
  • bunge huamua juu ya sheria
  • serikali inatekeleza sheria
  • mahakama zinaangalia utekelezaji na kuamua kama kuna mawazo tofauti
Vyombo vingine ni matawi mbalimbali ya serikali kulingana na katiba ya dola.
NGUZO KUU ZA SERIKALI
  1. serikali
  2. Mahakama
  3. Bunge
Vyombo hivi ni vyombo vya utendaji katika nchi,shughuli hizo ni kutekeleza utoaji wa haki,mamlaka ya  utendaji kutunga sheria na utekelezaji wa shughuli za umma.na kila chombo hutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa katiba.
SERIKALIUTAWALA
Ni chombo kinacho tekeleza madaraka ya utawala na chenye mamlaka kwa mujibu wa katiba,na serikali yetu hufuata misingi ya kidemokrasia na haki ya jamii.na wananchi ndio wenye mamalaka kamili na serikali huwajibika kwa wananchi na utekelezaji wa sera na mipango ya maendeleo ya nchi.
 Nguzo hii huundwa na  viogozi mbali mbali,kila kiongozi huyo huwa na shughuli zake tofauti za endaji katika serikali

RAIS


MAKAMU WA RAIS


BARAZA LA MAWAZIRI


WIZARA MBALAMBALI

WATUMISHI WA SERIKALI










 Soma na Eleza kazi za viongozi hao katika serikali










MAHAKAMA
Ni chombo cha kutafsiri sheria na kutoa haki kwa raia wote. mahakama ni muhimili au nguzo kuu ya tatu ya serikali.Mkuu wa muhimili huu ni jaji mkuu .
Ngazi ya mahakama Tanzania  ni kama zifuatazo:-
MAHAKAMA YA RUFAA

MAHAKAMA KUU

MAHAKAMA YA HAKIMU MKAZI/MKOA

MAHAKAMA YA WILAYA

MAHAKAMA YA MWANZO

 Kazi za mahakama
·         kulinda katiba na utawala wa sheria
·         Kulinda haki za raiya kama zilivyoainishwa katika katiba
·         Kutatua migogoro kati ya viombo vya dora
·         Kutatua migogoro baina ya raia wenyewe kwa wenyewe na kuwaadhibu wanao vunja sheria.
·         Kutoa uamuzi wa mwisho katika kutafsiri sheria  na kutafsiri sehemu za katiba zinazoleta utata.

BUNGE
Ni muhimili mkuu mwingine wa serikali.bunge huwekwa na watu ili litunge sheria na kusimamia serikali kwa niaba yao.Rais pia ni sehemu ya bunge.
Aina za wabunge
1.      Wabunge 232 waliochaguliwa kwenye majimbo wanayowakiisha
2.      Wabunge 5 kutoka baraza la wawakilishi Zanzibar
3.      Mwanasheria mkuu
4.      Wabunge wa viti maalum wanawake 20% ya wabunge wa majimbo
5.      Wabunge wa kuteuliwa na Rais(nafasi 10)

Tanzania Parliament consists of the following categories of members: (Article 66 of the Constitution)
  1. Members elected to represent constituencies.
  2. Women members whose number shall increase progressively starting with twenty per cent of the members named in sub-paragraphs (1), (3) and (4) of this paragraph, to be elected by the political parties that are represented in the National assembly in terms of Article 78 of the Constitution and on the basis of proportional representation amongst those parties.
  3. Five members elected by the Zanzibar House of Representatives from among its members,
  4. The Attorney General.
  5. Not more than ten members appointed by the President
The 2010 general elections produced the following numbers:



1.
Members elected from the same number of constituencies.
239
2.
Special seats women members.
102
3.
Members elected by the Zanzibar House of Representatives.
5
4.
Attorney General.
1
5.
Members appointed by the President.
10

Grand Total .
357



Kazi za bunge
  • To pass laws for the good governance.
  • To provide, by giving legislative sanction to taxation and acquisition
    of means to carrying out the work of the government.
  • To scrutinize government policy and administration, including
    proposal for expenditure; and to debate major issues of the day.
Kamati ya bunge
a)       Ulinzi na usalama
b)      Mambo ya nje
c)      Mashirika ya umma
d)     Huduma za jamii
e)      Kanuni za bunge
f)       Katiba na sheria
g)      Mazingira n.k
Viongozi wa bunge
  1. Spika na naibu spika
  2. Katibu wa bunge
  3. Waziri mkuu
  4. Kiongozi wa kambi ya  upinzani
NB

Mkuu wa dola (pia: Mkuu wa nchi) wa nchi ni kiongozi mwenye cheo kikuu. Lakini si lazima ya kwamba mkuu wa dola ana madaraka mengi sana. Hali inategemea na katiba ya nchi na utaratibu wake wa kisiasa. Pia si lazima ya kwamba nafasi ya mkuu wa dola inashikwa na mtu mmoja kwa sababu madaraka yake yanaweza kukabidhiwa pia kwa kamati ya viongozi.
Mkuu wa Dola katika Jamhuri
Katika mfumo wa jamhuri ya kisasa mkuu wa dola mara nyingi ni rais aliyechaguliwa na wananchi wote au na bunge.
Kimsingi kuna aina mbili za wakuu wa dola katika mfumo huu
  • rais ni mkuu wa nchi na pia mkuu wa serikali jinsi ilivyo Marekani, Tanzania na pia katika nchi nyingi za Afrika (serikali ya kiraisi).
  • rais ni mkuu wa nchi asiyeshughulika mambo ya serikali jinsi ilivyo Ujerumani au Uhindi (serikali ya kibunge) akiwa hasa mwakilishi mkuu wa taifa.
Katika mfumo wa pili rais anaweza kuwa na madaraka muhimu hasa wakati waziri mkuu au serikali iko matatani au baada ya uchaguzi. Mara nyingi rais huwa na kazi ya kumkabidhi kiongozi wa chama kikubwa wajibu wa kuanzisha serikali na kutafuta kibali cha wabunge. Lakini kama hakuna chama kikubwa baada ya uchaguzi au ahieleweki kiongozi yupi atafaulu kukusanya wabunge wengi kwa kuunda serikali kuna nafasi ya rais ya kumteua kiongozi na kumpa nafasi.
Mfumo wa tatu ulipatikana zaidi katika historia ni kamati kama mkuu wa dola. Siku hizi inapatikana katika Uswisi (viongozi 7 wa serikali wanaobadilishana kila baada ya mwaka), Bosnia na Herzegovina (marais 3 kutoka kila dola la shirikisho wanaobadilishana baada ya miezi 8) na jamhuri ya San Marino (maraisi 2 kwa pamoja wanoitwa "capitani reggenti"). Umoja wa Ulaya si dola kamili kwa hiyo hakuna mkuu wa dola lakini kuna uraisi unaoshikwa na serikali za mataifa wanachama yote kwa kubadilishana zamu za miezi 6.
Katika nchi nyingi rais ana pia nguvu ya veto juu ya sheria zilizopitishwa na bunge. Hii ni pamoja na nchi ambako sheria zote au sheria kadhaa zinapaswa kutiwa saini na rais baada ya kupitishwa na bunge. Rais akikataa azimio la bungo haiwi sheria. Ama inarudi bungeni au mahakama kuu inapaswa kutoa azimio.

Mkuu wa Dola katika Ufalme
Katika nchi zilizo chini ya muundo wa ufalme (pamoja na emirati, usultani au utemi) mkuu wa dola anaitwa mfalme au sultani n.k.
Hapa kuna pia viwango vya madaraka kwa mfalme vinavyofanana na nafasi ya rais katika jamhuri.
Katika historia mara nyingi wafalme walikuwa na madaraka makubwa sana wakiunganisha uongozi wa serikali pamoja na nafasi ya hakimu mkuu na pia madaraka ya kidini.
Siku hizi kuna wafalme wachache tu ambao ni watawala wanaoshika madaraka yote ya serikali na hawabanwi na katiba katika utekelezaji wa utawala wao. Mifano yake ni wafalme au masultani wa Saudia, Omani, Qatar, Uswazi, Brunei na Papa kama mkuu wa Dola la Vatikani.
Lakini wafalme wengi wako chini ya utaratibu wa katiba ya nchi na mara nyingi wana nafasi inayolingana na rais katika mfumo wa serikali ya kibunge. Katika nchi hizi sheria na maazimio ya mahakama yanaweza kutangazwa kwa "jina la mfalme" lakini hali halisi kiongozi mwenye madaraka makubwa ni waziri mkuu kama kiongozi wa serikali aliyechaguliwa au kuthebitishwa na wabunge wengi. Katika Ufalme wa Maungano (Uingereza) malkia inatangaza kila mwaka shabaha za serikali bungeni lakini hali halisi anasoma tu hotuba iliyoandikwa na waziri mkuu.

Katiba

Katiba ni sheria au kanuni zinazoanisha jinsi ambavyo nchi, chama, au shirika vitakavyoendesha shuguli zao. Kwa upande wa nchi, katiba ni sheria mama inayoainisha misingi mikuu ya kisiasa na kuonyesha madaraka na majukumu ya serikali. Katiba za nchi pia huanisha haki za msingi za wananchi.

Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Katiba kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Kuna aina kuu mbili za Katiba ambazo ni:

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

upimaji na tathimini

jipatie tablets,pc.i pad kwa bei ya punguzo zaidi

mapendezo ya utafiti

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA